M-Pesa kurahisisha zaidi malipo ya ving’amuzi

Ikiwa zimebaki siku chache kabla ya Mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA kusimamisha rasmi urushwaji wa matangazo ya analojia kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania inaamini kuwa huduma ya M-Pesa itabakia kuwa njia salama zaidi na ya kipekee itakayo wawezesha Watanzania popote walipo kulipia vifurushi vya vingamuzi vyao kwa urahisi na usalama zaidi.

Mkurugenzi mtendaji wa Vodacom Tanzania Rene Meza amesema kuwa anaamini urushwaji wa matangazo kwa njia ya digitali ni hatua moja ya maendeleo kwa taifa na kwamba Watanzania wasiwe na hofu ya sumbufu wa kupanga foleni ili kulipia huduma za televisheni kwa kuwa kila mmoja anaweza kufanya hivyo kutoka kiganja cha mkono wake kwa urahisi na haraka kupitia M-pesa wakati wowote na mahali popote.



“Dunia ya sasa inatumia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya Sayansi na teknolojia ili kurahisisha maisha ya watu wanaoishi humo, nasi tunapaswa kuhakikisha tunaendana na mabadiliko hayo, Vodacom itaendelea kuwa kiungo cha mbadiliko ya maisha ya ya watanzania kupitai teknolojia za simu.”

alisema Meza na kuongeza kuwa, “Katika mchakato huu wa kuhamia digitali kutoka anolojia huduma yetu ya M-pesa itasimama kuwa kiungo muhimu cha kuwaondolea wananchi kero ya kulipia huduma kila mwishoni mwa mwezi.

Meza aliongeza kuwa ni vyema sasa Watanzania wakatumia huduma ya M – Pesa kufanya malipo ya ving’amuzi vyao ili kuokoa muda na usumbufu ambao wanaweza kuupata kutokana na msongamano wa watu katika maeneo ya maouzo kwani ndio njia pekee rahisi na salama ambayo tayari imewawezesha wateja wake kufanya malipo hayo.

“Tunaamini katika kutoa suluhisho la kibiashara kwa wateja wetu, kwa wateja wenye ving’amuzi wanaohitaji kununua vifurushi kwa njia ya M-Pesa wanapaswa kupiga *150*00# na kisha kuchagua namba 4 Malipo, na kisha kuchagua 1 na kuweka namba ya kampuni na kuweka namba ya kumbukumbu ambayo iko katika king’amuzi chake, na kisha atachagua aina ya malipo anayotaka kufanya na kuingiza namba yake ya siri na kubonyeza 1 kuthibitisha,” alisema Meza.

Mpaka sasa mamlaka ya mawasiliano Tanzania imetoa vibali kwa kampuni zenye mamlaka ya kurusha matangazo kwa mfumo wa dijitali ambapo Star Media, Agape Assosiate Limited ambazo tayari zimekwisha ingia katika ushirikiano na kampuni ya Vodacom Tanzania kuwawezesha wateja wake kufanya malipo kupitia huduma ya M-Pesa.
Post Title : M-Pesa kurahisisha zaidi malipo ya ving’amuzi

M-Pesa kurahisisha zaidi malipo ya ving’amuzi,

M-Pesa kurahisisha zaidi malipo ya ving’amuzi

0 comments

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...